×
TAFUTA
Mahali Salama pa Kuchunguza Maswali
 jinsi unavyoweza kumjua Mungu
Kuunganishwa na Mungu

Kwa Nini Unaweza Kuamini Biblia

Ona ni nani aliandika Biblia na jinsi ilivyoandikwa. Ni historia ya Biblia inayoifanya iwe ya pekee sana kati ya ‘maandiko matakatifu.’

WhatsApp Share Facebook Share Twitter Share Share by Email More PDF

Sikiliza makala hii:

Historia ya Biblia - Nani aliandika Biblia?

Biblia iliandikwa kwa muda wa miaka 1500 na waandishi 40. Tofauti na maandishi mengine ya kidini, Biblia husomwa kama masimulizi ya habari ya kweli kuhusu matukio halisi, mahali, watu, na mazungumzo. Wanahistoria na wanaakiolojia wamethibitisha mara kwa mara ukweli wake.

Kwa kutumia mitindo ya waandishi wenyewe na haiba, Mungu anatuonyesha yeye ni nani na jinsi unavyoweza kumjua.

Kuna ujumbe mmoja mkuu unaobebwa kila mara na waandikaji wote 40 wa Biblia: Mungu, aliyetuumba sisi sote, anatamani kuwa na uhusiano nasisi. Anatuita tumjue na kumwamini.

Biblia haitutii moyo tu, inatueleza maisha na Mungu kwetu. Haijibu maswali yote ambayo tunaweza kuwa nayo, lakini inatutosha kabisa. Inatuonyesha jinsi ya kuishi kwa kusudi na kwa wema. Jinsi ya kujihusisha na wengine. Inatutia moyo tumtegemee Mungu ili kupata nguvu, mwongozo, na kufurahia upendo wake kwetu. Biblia pia inatuambia jinsi tunavyoweza kupata uzima wa milele.

Vitengo vingi vya uthibitisho vinaunga mkono usahihi wa kihistoria wa Biblia na vilevile madai yake ya uandishi wa kimungu. Hapa kuna sababu chache ambazo unaweza kuiamini Biblia.

Akiolojia inathibitisha kwa usahihi wa kihistoria ya Biblia.

Wanaakiolojia wamegundua mara kwa mara majina ya maofisa wa serikali, wafalme, majiji, na sherehe zinazotajwa katika Biblia -- nyakati fulani wakati wanahistoria hawakufikiri kuwa watu kama hao au maeneo kama hayo yalikuwepo. Kwa mfano, Injili ya Yohana inaeleza juu ya Yesu kuponya kiwete karibu na Bwawa la Bethzatha. Maandishi yanaelezea hata milango mitano (njia za miguu) zinazoelekea kwenye bwawa. Wasomi hawakufikiri kwamba bwawa hilo lilikuwepo, hadi wanaakiolojia walipolikuta likiwa na futi arobaini chini ya ardhi, likiwa limekamilika na milango mitano.1

Biblia ina maelezo mengi sana ya kihistoria, kwa hiyo si kila kitu kilichotajwa ndani yake bado kimepatikana kupitia akiolojia. Hata hivyo, hakuna ugunduzi wowote wa kiakiolojia ambao umepingana na yale ambayo Biblia imeyaifadhi.2

Tofauti na hilo, mwandishi wa habari, Lee Strobel alisema hivi kuhusu Kitabu cha Mormon: “Akiolojia imeshindwa mara kwa mara kuthibitisha madai hayo kuhusu matukio ambayo yanadaiwa yalitokea zamani sana katika Amerika. Ninakumbuka andiko nililoandika kwenda kwa taasisi ya Smithsonian kuuliza kwamba kama wameweza kupata udhibitisho wa madai ya Umomoni, ili tu kudhibitishiwa kwamba waakiolojia waliona nini katika habari za umomoni ‘hakuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya akiolojia ya Ulimwengu Mpya na mada inayozungumziwa katika kitabu hicho.’” Waakiolojia hawajapata kamwe kupata majiji, watu, majina, au mahali palipotajwa. Katika Kitabu cha Mormoni.3

Maeneo mengi ya kale yaliyotajwa na Luka, katika Kitabu cha Matendo ya Mitume katika Agano Jipya, yametambuliwa kupitia akiologia. “Kwa ujumla, Luka anazitaja nchi thelathini na mbili, miji hamsini na minne na visiwa tisa bila kosa.”4

Akiolojia pia imekanusha nadharia nyingi zisizo na msingi kuhusu Biblia. Kwa mfano, nadharia ambayo bado inafundishwa katika vyuo fulani leo inadai kwamba Musa hangeweza kuandika Pentateuki (yaani vitabu vitano vya kwanza vya Biblia), kwa sababu uandishi haukuwa umebuniwa katika siku zake. Kisha wanaakiolojia waligundua Black Stele. “Ilikuwa na herufi zenye umbo la kabari juu yake na ilikuwa na sheria za kina za Hammurabi. Je, ilikuwa baada ya Musa? Hapana! Ilikuwa kabla ya Musa; si hivyo tu, bali ilikuwa kabla ya Ibrahimu (2,000 K.K). Ilitangulia maandishi Musa kwa karne tatu hivi.”5

Akiolojia inadhibitisha kwa uhakika historia ya usahihi wa Biblia.

Bonyeza hapa kuona chati yenye orodha ya baadhi vitu vikuu vya kiakiolojia vilivyogunduliwa

Biblia tulionayo leo ni sawa na ile iliyoandikwa mwanzoni.

Baadhi ya watu wana wazo kwamba Biblia imetafsiriwa “mara nyingi sana” hivi kwamba imepotoshwa kupitia hatua za kutafsiri. Labda hiyo ingekuwa kweli ikiwa tafsiri hizo zingefanywa kutoka kwa tafsiri zingine. Lakini tafsiri zinafanywa moja kwa moja kutoka kwa maandishi asilia ya Kigiriki, Kiebrania na Kiaramu kulingana na maelfu ya maandishi ya kale.

Usahihi wa Agano la Kale la leo ulithibitishwa mwaka wa 1947 wakati wataalamu wa vitu vya kale walipopata “Magongo ya Bahari ya Chumvi” kando ya Ukingo wa Magharibi wa Israeli leo. “Gombo la Bahari ya Chumvi” lilikuwa na maandiko ya Agano la Kale yenye umri wa miaka 1,000 kuliko maandishi yoyote tuliyokuwa nayo. Tunapolinganisha maandishi yaliyopo na haya, kutoka miaka 1,000 mapema, tunapata makubaliano 99.5% ya wakati huo. Na tofauti za .5% ni tofauti ndogo za tahajia na muundo wa sentensi ambao haubadilishi maana ya sentensi.

Kuhusu Agano Jipya, ni hati ya kale inayotegemewa zaidi na wanadamu.

Maandishi yote ya kale yaliandikwa kwenye mafunjo au magamba ya miti au karatasi nene, ambayo haikuwa na maisha mengi ya rafu. Kwa hivyo watu walinakili maandishi asili kwa mkono, ili kudumisha ujumbe na kuusambaza kwa wengine.

Watu wachache wanatilia shaka uandishi wa Plato wa “Jamhuri”. Ni wa zamani sana, maana uliyoandikwa na Plato karibu mwaka wa 380 K.K. Nakala za mwanzo kabisa tulizo nazo ni za mwaka wa 900 K.K., ni sawa na kipindi cha miaka 1,300 tangu alipoiandika. Na mpaka sasa tuna nakala saba tu zilizopo.

“Vita vya Gallic” vya Kaisari viliandikwa karibu miaka ya 100 - 44 K.K. Nakala tulizo nazo leo ni za miaka 1,000 baada ya kuziandika. Kati ya hizo tuna nakala kumi.

Linapokuja suala la Agano Jipya, lililoandikwa kati ya 50 -100 B.K, kuna zaidi ya nakala 5,000. Zote ziko ndani ya miaka 50-225 ya uandishi wao wa asili. Zaidi ya hayo, ilipokuja suala la maandiko, waandishi (watawa) walikuwa waangalifu sana katika kunakili na zilizoandikwa kwa mkono asilia. Waliangalia na kukagua tena kazi yao, ili kuhakikisha inalingana kabisa. Yale ambayo waandishi wa Agano Jipya waliandika awali yamehifadhiwa vizuri zaidi kuliko hati nyingine yoyote ya kale. Tunaweza kuwa na hakika zaidi ya kile tunachosoma kuhusu maisha na maneno ya Yesu, kuliko tunavyo hakika na maandishi ya Kaisari, Plato, Artistotle na Homer.

Kwa ulinganisho wa Agano Jipya na maandishi mengine ya kale, bonyeza hapa.

Sababu zaidi za kuamini utunzi wa injili za Yesu.

Waandishi wanne wa Agano Jipya kila mmoja aliandika wasifu wake juu ya maisha ya Yesu. Hizi zinaitwa injili nne, vitabu vinne vya kwanza vya Agano Jipya. Wanahistoria wanapojaribu kubainisha ikiwa wasifu ni wa kutegemewa, wanauliza, “Ni vyanzo vipi vingine vinavyoripoti maelezo sawa kuhusu mtu huyu?”

Hivi ndivyo hii inavyofanya kazi. Fikiria unakusanya wasifu wa Rais John F. Kennedy. Unakuta wasifu mwingi ukielezea familia yake, urais wake, lengo lake la kumweka mtu mwezini, na jinsi alivyoshughulikia Mgogoro wa Kombora la Cuba. Kuhusu Yesu, je, tunaweza kupata vitabu vingi vya wasifu vinavyoripoti mambo sawa kuhusu maisha yake? Ndiyo. Hapa kuna mifano ya ukweli kuhusu Yesu, na ambapo unaweza kupata ukweli huo ukiripotiwa katika kila moja ya wasifu wao.

  Mathayo Marko Luka Yohana
Yesu alizaliwa na bikira 1:18-25 - 1:27, 34 -
Yesu alizaliwa mjini Bethlehemu 2:1 - 2:4 -
Yesu aliishi Nazareti 2:23 1:9, 24 2:51, 4:16 1:45, 46
Yesu alibatizwa na Yohana mbatizaji   3:1-15 1:4-9 3:1-22 -
Yesu alifanya miujiza mingi ya uponyaji 4:24, etc. 1:34, etc. 4:40, etc. 9:7
Yesu alitembea juu ya maji 14:25 6:48 - 6:19
Yesu aliwalisha watu 5000 kwa
mikate mitano na samaki wawili.
14:7 6:38 9:13 6:9
Yesu alifundisha watu wa kawaida 5:1 4:25, 7:28 9:11 18:20
Yesu alitumia muda kukaa na watu waliotengwa na jamii 9:10, 21:31 2:15, 16 5:29, 7:29 8:3
Yesu alibishana na viongozi wa dini 15:7 7:6 12:56 8:1-58
Viongozi wa dini walipanga njama ya kumuua 12:14 3:6 19:47 11:45-57
Walimkabidhi Yesu kwa Warumi   27:1, 2 15:1 23:1 18:28
Yesu alipigwa mijeledi 27:26 15:15 - 19:1
Yesu alisulubishwa 27:26-50 15:22-37 23:33-46 19:16-30
Yesu alizikwa kaburini 27:57-61 15:43-47 23:50-55 19:38-42
Yesu alifufuka kutoka katika wafu na
akawatokea wafuasi wake
28:1-20 16:1-20 24:1-53 20:1-31

Wasifu wa injili mbili ziliandikwa na mitume Mathayo na Yohana, wanaume hawa waliomjua Yesu kibinafsi na walisafiri pamoja naye kwa zaidi ya miaka mitatu. Vitabu vingine viwili viliandikwa na Marko na Luka, washiriki wa karibu wa mitume. Waandishi hawa walikuwa na ufikiaji wa moja kwa moja wa ukweli ambao walikuwa wakiutunza. Wakati wa kuandikwa kwao, bado kulikuwa na watu waliokuwa hai waliokuwa wamemsikia Yesu akisema, walimwona akiponya watu na kufanya miujiza.

Kwa hiyo kanisa la kwanza lilikubali Injili nne kwa urahisi kwa sababu walikubaliana na yale ambayo tayari yalikuwa maarifa ya kawaida kuhusu maisha ya Yesu.

Kila injili ya Mathayo, Marko, Luka na Yohana, inasomwa kama ripoti za habari, hesabu ya kweli ya matukio ya siku, kila moja kutoka kwa mtazamo wake. Maelezo ni ya kipekee kwa kila mwandishi, lakini ukweli unapatana.

Kwa mfano unaotoka kwenye mojawapo ya Injili, bonyeza hapa.

Hii ndio sababu injili ziliandikwa.

Katika miaka ya karibuni baada ya kifo na ufufuo wa Yesu hapakuwa na haja ya wazi ya kuandika wasifu kuhusu Yesu. Wale walioishi katika eneo la Yerusalemu walikuwa mashahidi wa Yesu na walijua vyema huduma yake.6

Hata hivyo, habari za Yesu zilipoenea nje ya Yerusalemu, na mashahidi waliojionea hawakupatikana tena kwa urahisi, kulikuwa na uhitaji wa masimulizi yaliyoandikwa ili kuwaelimisha wengine kuhusu maisha na huduma ya Yesu.

Ikiwa ungependa kujua zaidi kuhusu Yesu, makala hii itakupa muhtasari mzuri wa maisha yake: Kwa nini Yesu ni Mungu.

Jinsi vitabu vya Agano Jipya viliamuliwa.

Kanisa la kwanza lilikubali vitabu vya Agano Jipya mara tu vilipoandikwa. Tayari imetajwa kwamba waandishi walikuwa marafiki wa Yesu au wafuasi wake wa karibu, wanaume ambao Yesu alikuwa amewakabidhi uongozi wa kanisa la kwanza. Waandikaji wa Injili Mathayo na Yohana walikuwa baadhi ya wafuasi wa karibu zaidi wa Yesu. Marko na Luka walikuwa ni wafuasi wa karibu na mitume, walikuwa na uwezo wa kupata masimuzi maisha ya Yesu kupitia kwa mitume.

Waandishi wengine wa Agano Jipya waliokuwa na uwezo kumfikia Yesu ni Yakobo na Yuda walikuwa ndugu wa kambo wa Yesu ambao mwanzoni hawakumwamini. Na Petro alikuwa mmoja wa wale mitume 12. Na kwa upande wa Paulo alianza akiwa mpinzani mkali wa Ukristo na mshiriki wa jamii inayoongoza ya kidini, lakini akawa mfuasi mwenye bidii wa Yesu, akiwa na hakika kwamba Yesu alifufuka kutoka kwa wafu.

Ripoti katika vitabu vya Agano Jipya zilifuatana na kile ambacho maelfu ya watu walikuwa wamejionea wenyewe. Vitabu vingine vilipoandikwa mamia ya miaka ya baadaye, haikuwa vigumu kwa kanisa kuviona kuwa vya kughushi. Kwa mfano, Injili ya Yuda iliandikwa na madhehebu ya Kinostiki, karibu 130 - 170 W.K., muda mrefu baada ya kifo cha Yuda. Injili ya Tomaso, iliyoandikwa karibu 140 A.D., ni mfano mwingine wa maandishi ghushi yenye jina la mitume kimakosa. Injili hizi na nyinginezo za Kinostiki zilipingana na mafundisho yanayojulikana ya Yesu na Agano la Kale, na mara nyingi zilikuwa na makosa mengi ya kihistoria na kijiografia.7

Mnamo 367 B.K., Athanasius aliorodhesha rasmi vitabu 27 vya Agano Jipya (orodha ile ile tuliyo nayo leo). Muda mfupi baadaye, Jerome na Augustine walisambaza orodha hiyohiyo. Orodha hizi, hata hivyo, hazikuwa za lazima kwa Wakristo walio wengi. Kwa kiasi kikubwa kanisa zima lilikuwa limetambua na kutumia orodha hiyo ya vitabu tangu karne ya kwanza baada ya Kristo.

Kadiri kanisa lilivyokua zaidi ya nchi zinazozungumza Kigiriki na kuhitaji kutafsiri Maandiko, na madhehebu yaliyogawanyika yalipoendelea kutokeza na vitabu vyao vitakatifu vilivyoshindana, ikawa muhimu zaidi kuwa na orodha mahususi.

Wanahistoria wanathibitisha yale ambayo Biblia inasema kumhusu Yesu.

Sio tu kwamba tuna nakala zilizohifadhiwa vizuri za maandishi ya asili, pia tuna ushuhuda kutoka kwa wanahistoria wa Kiyahudi na Kirumi.

Injili zinaripoti kwamba Yesu wa Nazareti alifanya miujiza mingi, aliuawa na Warumi, na kufufuka kutoka kwa wafu. Wanahistoria wengi wa kale wanaunga mkono ujumbe wa Biblia kuhusu maisha ya Yesu na wafuasi wake:

Cornelius Tacitus (mwaka 55-120 BK), mwanahistoria wa Roma karne ya kwanza, anachukuliwa kuwa mmoja wa wanahistoria sahihi zaidi wa ulimwengu wa kale.8 Walioitwa Wakristo ... [Kristo], ambaye jina lilitokana naye, alikabiliwa na adhabu kali sana wakati wa utawala wa Tiberio mikononi mwa mmoja wa watawala wetu, Pontio Pilato.…”9

Flavius Josephus, mwanahistoria Myahudi (A.D. 38 - 100), aliandika kuhusu Yesu katika kitabu chake cha Jewish Antiquities. Kutoka kwa Josephus, “tunajifunza kwamba Yesu alikuwa mtu mwenye busara ambaye alifanya mambo ya kushangaza, alifundisha wengi, alishinda wafuasi waliotoka kwa Wayahudi na Wagiriki, aliaminika kuwa Masihi, alishtakiwa na viongozi wa Kiyahudi, alihukumiwa kusulubiwa na Pilato na alihesabiwa kuwa amefufuliwa.”10

Suetonius, Pliny Mdogo, na Thallus pia waliandika kuhusu ibada ya Kikristo na mateso ambayo yanapatana na masimulizi ya Agano Jipya.

Hata sheria na tamaduni za Kiyahudi zilizokusanywa na kuandikwa (Talmud), kwa hakika hazina upendeleo wa kumwelekea Yesu, zinakubaliana kuhusu matukio makuu ya maisha yake. Kutoka kwa kwahizo sheria na tamaduni za kiyaudi zilizoandikwa, “tunajifunza kwamba Yesu alitungwa mimba nje ya ndoa, akakusanya wanafunzi, akatoa madai ya kufuru juu yake mwenyewe, na kufanya miujiza, lakini miujiza hii inahusishwa na uchawi na si kwa Mungu.”11

Hii ni habari ya kushangaza tukizingatia kwamba wanahistoria wengi wa kale walikazia fikira viongozi wa kisiasa na kijeshi, si waalimu wasiojulikana kutoka mikoa ya mbali ya Milki ya Roma. Hata hivyo wanahistoria wa kale (Wayahudi, Wayunani na Warumi) wanathibitisha matukio makubwa ambayo yanawasilishwa katika Agano Jipya, ingawa hawakuwa waamini wenyewe.

Je, inajalisha ikiwa kweli Yesu alifanya na kusema yaliyo katika Injili?

Ndiyo. Ili imani iwe ya thamani yoyote, ni lazima itegemee mambo ya hakika, juu ya ukweli. Hii ndio sababu. Ikiwa unasafiri kwa ndege kwenda London, labda ungekuwa na imani kwamba ndege hiyo ina nguvu na inategemeka kiufundi, rubani amepata mafunzo, na hakuna magaidi ndani yake. Imani yako, hata hivyo, sio inayokupeleka London. Imani yako ni muhimu kwa kuwa ilikupata kwenye ndege. Lakini kinachokupeleka London ni uzima wa ndege, uwezo wa rubani, n.k. Unaweza kutegemea uzoefu wako mzuri wa safari za ndege zilizopita. Lakini uzoefu wako mzuri haungetosha kupata ndege hiyo ya London. Kinacho jalisha na cha muhimu ni lengo la imani yako – iwe ya kuaminika?

Je, Agano Jipya ni uwasilishaji sahihi na unaoamiwa wa Yesu? Ndiyo. Tunaweza kuliamini Agano Jipya kwa sababu kuna uungwaji mkono mkubwa sana wa kweli kwa hilo Agano Jipya. Makala hii iligusia mambo yafuatayo: wanahistoria wanakubaliana, waakiolojia nao wanakubaliana, wasifu wa Injili nne unapatana, uhifadhi wa nakala za hati ni wa ajabu, kuna usahihi wa hali ya juu katika tafsiri. Yote haya yanatoa msingi thabiti wa kuamini kwamba kile tunachosoma leo ndicho ambacho waandishi wa awali waliandika na uzoefu katika maisha halisi, katika maeneo halisi.

Yohana, mmoja wa waandishi anahitimisha vizuri, “Basi Yesu alifanya ishara nyingine nyingi mbele ya wanafunzi wake, zisizoandikwa katika kitabu hiki; lakini hizi zimeandikwa ili mpate kuamini ya kwamba Yesu ndiye Kristo Mwana wa Mungu, na kwa kuamini muwe na uzima kwa jina lake.”12

 Jinsi ya kuanza uhusiano na Mungu
 Nina swali…

Maelezo ya Chini: (1) Strobel, Lee. Kesi ya Kristo (Zondervan Publishing House, 1998), uk.132. (2) Mwanaakiolojia mashuhuri wa Kiyahudi, Nelson Glueck, aliandika: “Inaweza kusemwa waziwazi kwamba hakuna uvumbuzi wa kiakiolojia ambao umewahi kupinga marejeo ya Biblia.” Nelson Glueck, Mito katika Jangwa: Historia ya Negev. Jewish Publication Society of America, Philadelphia, 1969, P. 176. (3) Strobel, p. 143-144. (4) Geisler, Norman L. Baker Encyclopedia of Christian Apologetics (Grand Rapids: Baker, 1998). (5) McDowell, Josh. Ushahidi Unaodai Hukumu (1972), uk. 19. (6) Ona Matendo 2:22, 3:13, 4:13, 5:30, 5:42, 6:14, n.k. (7) Bruce, F.F. The Books and the Parchments: How We Got Our English Bible (Fleming H. Revell Co., 1950), p. 113. (8) McDowell, Josh. Ushahidi Mpya Unaodai Hukumu (Thomas Nelson Publishers, 1999), p. 55. (9) Tacitus, A. 15.44. (10) Wilkins, Michael J. & Moreland, J.P. Jesus Under Fire (Zondervan Publishing House, 1995), p. 40. (11) Ibid. (12) Yohana 20:30, 31


SHIRIKISHA WENGINE
WhatsApp Share Facebook Share Twitter Share Share by Email More